Sunday 9 October 2011

Teknolojia ni chombo muhim cha maendeleo sio luxury



(Angalizo: Kwenye article hii nitatumia neno IT na ICT kumaanisha kitu kimoja)
Penda usipende teknolojia imeleta mapinduzi makubwa sawasawa na wakati wa industrial revolution. Nchi nyingi zimepiga hatua kubwa kwa kuona umuhim wa kuwekeza kwenye sekta hii. Makampuni kama Amazon.com yamechukua full advantage of IT kutengeneza mamilion ya hela, kutoa huduma kwa jamii na kuajiri maelfu. Hata hivyo kusuasua na kusita kuwekeza kwenye teknolojia kumedhoofisha nchi nyingi na makampuni mengi.

Japokuwa hali ya uchumi wa dunia unayumba sana, watu wakiishi kwa hofu na mashaka, ni muhimu kuendelea kuhimiza uwekezaji kwenye sekta ya teknolojia. Viongozi katika sekta mbalimbali wamekuwa wakiona IT kama kitu ambacho ni kizuri kuwa nacho lakini sio muhimu sana. Kwa sababu hiyo imani imejengeka kwamba unawekeza zaidi kwenye IT pale unapokuwa kwenye hali nzuri kiuchumi na kuacha ama kutokuipa ICT umuhimu pale mambo ya kiuchumi yanapotetereka. ICT imekuwa victim kila inapotokea bajeti imeyumba.

Kwa kuendelea kuona kwamba IT au ICT sio chombo muhimu cha maendeleo, nchi na jamii zetu zimekuwa zikishindwa kuendana na kasi ya teknolojia. Hata tunapotaka sasa kuwekeza kwenye sekta hii wakati mambo yanapokuwa mazuri kidogo tunakuwa tumeachwa nyuma sana.

Kuwekeza kwenye ICT kunahusisha mambo makuu mawili:
1. Research in technology - hii ina-stimulate innovation
2. ICT/IT consumption - hii inahusisha education; infrastructures; hardware and software acquisation; n.k

Tunawahimiza viongozi kwenye private as well as public sector kubadilika na kujifunza kutoka kwa wengine. Inawezekana bajeti haitoshi, lakini kwa kui-sacrifice ICT ama kutokuona umuhimu wake ni vigumu ku-compete kwenye hii dunia ya leo.
Tunapenda kusisitiza kwamba ICT sio luxury bali chombo muhimu cha maendeleo. Tuendelee kuhimiza uwekezaji kwenye sekta ya teknolojia

2 comments:

emuthree said...

Ni kweli hilo, tupo pamoja

Anonymous said...

Tunahitaji kuwaelimisha mameneja wa kizamani wanaturudisha nyuma huku makazini. I hope they read this article.

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

 
Design by Goodluck Mboya | Bloggerized by IT4Dev - Premium Design